Dr Ali Mohmed Sheni amewakemea wanoutaka uongozi kwa kutumia misikiti Unguja.

 
 
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Alhaj Dr Ali Mohmed Shein amewakemea wanaotafuta uongozi kwa kutumia misikiti na kusema kitendo hicho ni kinyume na maadili ya dini ya kiislamu.

Dr Shein ametioa kauli hiyo huko Makunduchi wilaya ya kusini Unguja wakati akiongea na waumini wa kiislamu baada ya kuuzindua na kuufungua msikiti mpya uliojengwa kwa nguvu za wananchi na kushirikaina na wafadhili ambapo amesema msikiti ni nyumba ya ibada nasio mahali pa kutafuta umaarufu au uongozi na sehemu hiyo iheshemiwe nasiyo mahali pa mivutano na migogoro.
 
Mbali yakuufungua msikiti Alhaj Dr Shein baadaye alapata fursa ya kufungua madrasaa ya kisasa iliyojengwa huko kiungoni ambayo inatarajiwa kutoa elimu ya dini na kijamii kwa watoto wa Makunduchi ambapo aliwataka wazeee kuwa karibu na vijana wao nasio kuwachiasuala la elimu kwa waalimu pekee kwa vile watoto hao ni tegemeo kubwa la baadaye, kwa upande wake waziri wa kazi na utumishi wa umma ambaye pia ni mwaklishi wa jimbo hilo Mhe Haroun Ali Suleiman amesema ujenzi wa msikiti na madrasaa umewezekana kutoakana na umoja wa wananchi walionyesha kwa wafadhili. 
 
Msikiti huo ambao upo tokea miaka zaidi ya miaka 100  na ujenzi wa madrassa huku ikiwa ni harakati za uongozi wa jimbo hilo kuhakiksiha vijana wanpata elimu wakiwa karibu na maeneo ya makaazi badala ya kuhangaika na kutembea maneo ya mbali.

0 comments: