Wafugaji waiomba serikali kuangalia namna ya kuweza kudhibiti wahalifu na wahamiaji haramu loliond

 
 
Wananchi wa jamii za wafugaji wa kata ya ololosokwani iliyoko tarafa ya loliondo wilayani ngorongoro mkoani  arusha wameiomba serikali kusaidia kudhibiti wahalifu  na wahamiaji haramu wanaotumia vibaya fursa za ujirani  mwema kukiuka sheria za nchi.

Wananchin hao wamemweleza mkuu wa mkoa wa arusha  Bw.Felexs Ntebenda kijiko aliyetmbelea eneo hilo kuwa  pamoja na kuwepo kwa ushirikiano  mzuri  na wenzao wa nchi jirani hasa  wakati  matatizo yakiwemo ya  kiangazi baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya fursa hiyo  ikiwa ni pamoja na kugoma kurudi makwao.
 
Wazee wa mila wa kabila hilo wamesema hadi sasa hakuna  tatizo lolote kwani wanaendelea kudumisha amani kwa  kutumia viongozi wao wa mila wenyeviti wa mitaa na  mabalozi wa nyumba kumi lakini hali inavyokwenda   wanahitaji msaada wa vyombo vya dola.
 
Kufuatia malalamiko hayo mkuu wa mkoa Bw.Ntebenda  amesema serikali itajenga kituo kikubwa cha polisi na ofisi ya uhamiaji katika eneo hilo ili sheria ziweze  kufuatwa.

0 comments: